?> HISTORIA STANDARD FOUR EXAMS SERIES
HISTORIA STANDARD FOUR EXAMS SERIES

Jina La Mwanafunzi: _____________________________________
Jina La Shule:_____________________________________

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA WAZIRI MKUU -TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

 MTIHANI WA MUHULA WA KWANZA DARASA LA TANO

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

Muda: saa 1:30 MEI 2026

 SEHEMU A (Alama 20) 

i. Kupendana huleta amani na kuwajali watu wengine pia,Ni kitendo gani kati ya vifuatavyo sio sahihi kuwatendea wenzetu? 

A. kuwasaidia B. Kushauriana nao C. Kuaminiana D. kuwadhulumu E. kushirikiana ( )

ii. Hapo kale Nchi nyingi za kiafrika zilitawaliwa na mataifa ya kigeni,Je, Hali ya nchi moja kuitawala nchi nyingine kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni inaitwaje? 

A. Ubepari B. Ujamaa C. ukoloni D. uzalendo E. utumwa ( ) 

iii. Viwanda vingi wakati wa ukoloni vilianzishwa hasa kwa ajili ya kuchakata nini? 

A. Mazao B. Mkonge C. Tumbaku D. Madini E. Malighafi ( ) 

iv. Ipi kati ya zifuatazo sio sekta ya uchumi wakati wa ukoloni wa waingereza? 

A. kilimo B. viwanda C. madini D. biashara E. afya ( )

v. Kiongozi aliyeongoza jamii ya wahehe kupambana na uvamizi wa wajerumani alikuwa nani?

A. Mkwawa B. Machemba C. Mangi Sina D. Abushiri E. Isike ( ) 

vi. Mtu aliyepewa dhamana ya kusimamia vibarua wakifanya kazi katika mashamba ya wakoloni alijulikana kama nani? A.Akida B.Jumbe C.Mnyapara D.Liwali E.Gavana ( )

vii. Sayansi na teknolojia ya asili ya kutengenezea moto iligundulika katika kipindi kipi cha zama za mawe? 

A. zama za mawe za kati B. zama za mawe za kale C. zama za mawe za mwisho D. zama za chuma E.Zama za mawe za chuma ( )

viii.Ni ngazi ipi katika uongozi wa shule huongozwa na wazazi ambao huchaguliwa na wazazi wenye watoto katika shule husika? 

A. Kamati ya shule B. Mwalimu wa Taaluma C. mwalimu wa nidhamu D. Mwalimu mkuu E. kiranja mkuu ( ) 

ix. Urithi wa historia inayohusu michoro ya mapangoni unapatikana sehemu gani kati ya hizi zifuatazo? 

A. Isimila Iringa B. Kondoa Irangi C. Bonde la Ngorongoro D. Olduvai Arusha E.Laetoli Arusha ( )

x. Mwanamama mahiri na shupavu aliyejulikana kama Litti Kidanka ambaye alionesha upinzani mkubwa dhidi ya Wajerumani alikuwa wa kabila gani kati ya haya yafuatayo? 

A. Wagogo B. Wanyeramba C. Wangoni D. Wanyaturu E. Wamasai ( )

2. Oanisha mwaka kutoka orodha A na tukio husika kutoka orodha B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi kwenye mabano.

Orodha A

Majibu

Orodha B

i. 1890


A. Vita vya Maji Maji

B. Kuteuliwa kwa Donald Cameroon

C. Kusainiwa kwa mkataba wa Heligoland

D. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

E. Jina Tanganyika lilizaliwa

F. Kifo cha Abeid Amani Karume

G. Kifo cha baba wa taifa Mwl. J. K Nyerere

ii. 1964


iii. 1905 - 1907


iv. 1999


v. 1920


 3. Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kuchagua jibu sahihi kutoka kwenye mabano uliyopewa.

i. Mambo ya lazima ambayo mtu hupaswa kuyatenda ili kukabiliana na mazingira yanayomzunguka huitwaje …………………………………...… (haki/wajibu)

ii. Mwaka 1954 chama cha TAA kiliitisha mkutano mkuu kujadili katiba na muundo wake, ambapo katika mkutano huo kulizaliwa chama kipya cha siasa kilichojulikana kama.....................(CCM/TANU)

iii. ………………………………........................ ni miongoni mwa athari chanya za mfumo wa elimu ya kikoloni. (Kuua lugha za asili/Kueneza lugha ya Kiswahili)

iv. Sheria na kanuni zinazoainisha jinsi nchi itakavyoendeshwa huitwa

…………………………………………. (katiba/kitabu)

v. Ujio wa ..................................ulichochea mabadiliko makubwa katika maadili ambayo ni dini ya Kiislam na biashara ya utumwa. (Wajerumani/Waarabu)

 SEHEMU B (Alama 20)

4. Umepewa ngazi 4 za uongozi katika serikali ya Wajerumani ambazo hazipo katika mpangilio sahihi. Zipange ngazi hizo kuanzia ngazi ya juu Kwenda chini kwa kuandika herufi ya jibu sahihi.

Mpangilio usio sahihi

Mpangilio sahihi

A. Gavana

i.

B. Waziri wa makoloni

ii.

C. Baraza la kumshauri Gavana

iii.

D. Liwali

iv.

E. Afisa Wilaya

v.



5. Chunguza picha ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata.

image 

Maswali 

i. Mnyama huyo hutumika kama alama ya Taifa, je, anaitwaje?

_____________________________________

ii. Alama hiyo ya Taifa ni kiashiria cha uwepo wa nini nchini Tanzania? 

_____________________________________

iii. Taja chombo cha usafiri kinachomilikiwa na serikali ya Tanzania ambacho picha ya mnyama huyo huwekwa kama Ishara ya kuonesha kuwa ni mali ya Tanzania 

_____________________________________

iv. Mnyama huyu hutumika kama alama ya mficho kwenye

_____________________________________

v. Taja alama za Taifa nyingine mbili (2) unazozifahamu

 A)_____________________________________

B)_____________________________________

 SEHEMU C (Alama 10)

 6.Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.

Uzalendo ni hali ya mtu kuwa na moyo wa kuipenda na hata kuwa tayari kuifia nchi yake.Uzalendo unajumuisha kuipenda nchi yako kwa kuithamini na kuilinda.Wanamichezo huonesha uzalendo wao pale wanapoipeperusha Bendera ya Taifa lao katika mataifa mengine sambamba na kuimba wimbo wa Taifa lao.Uzalendo hauigizwi bali ni hisia kali za mapenzi kwa nchi kutoka ndani ya moyo mwa raia mwaminifu na mtiifu. Uzalendo upo kwa kila mwananchi anayejitambua na kujithamini pia. Hata hivyo kila mmoja wetu katika nafasi yake anapaswa kuwa mzalendo. Serikali huhimiza viongozi na wananchi kuwa wazalendo na kuzingatia maslahi ya Taifa badala ya maslahi binafsi na kwa kufanya hivyo itapunguza tamaa ya kujilimbikizia mali. Kwa maana hiyo mwananchi anayeipenda Tanzania kwa dhati ya moyo wake, hataweza kushiriki vitendo vya rushwa kamwe.

 Maswali

i. Hali ya mtu kuwa na moyo wa kuipenda na hata kuwa tayari kuifia nchi yake huitwa

 _____________________________________

ii. Taja viashiria viwili vinavyotumiwa na wanamichezo kuonesha uzalendo kwa nchi yao wawapo katika mataifa mengine

(a)_____________________________________

(b) _____________________________________

iii. Uzalendo haugizwi, je unatoka kwenye moyo wa raia mwenye sifa gani?

_____________________________________

iv. Serikali inahimiza uzalendo na kuzingatia maslahi ya Taifa ili kukwepa nini?

_____________________________________

v. Kuipenda nchi yako kwa moyo wako kunakuepusha na vitendo gani?

_____________________________________

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD FOUR EXAM SERIES 132

Jina La Mwanafunzi: _______________________________________
 Jina La Shule: ___________________________________________

JAMIHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA

MTIHANI WA MUHULA WA MWEZI MEI 2026

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI DARASA LA IV

MAELEKEZO

  1. Mtihani huu una sehemu A, B na C zenye maswali 5 na vipengele 25.
  2. Jibu maswali yote.
  3. Fuata maelekezo yote uliyopewa katika kila swali.
  4. Andika jina lako, la shule na halmashauri kwenye sehemu wazi hapo juu.
  5. Maandishi yote yaandikwe kwa kalamu ya wino wa bluu au mweusi.
  6. Vifaa vya mawasiliano na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani

SEHEMU A (ALAMA 30)

1. Chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi hiyo katika mabano.

i. Nini kinachoelezea kuhusu Maisha yetu binafsi, familia, jamii inayotuzunguka, nchi au dunia?

  1. Matukio
  2. Historia. [ ]
  3. Mazingira
  4. Maisha

ii. Kila mtoto katika jamii ana haki stahiki anazopaswa kuzipata. Je ni haki ipi ya mtoto humwezesha kupata maarifa na ujuzi utakaomwezesha kuchangia maendeleo yake na jamii kwa ujumla? 

  1. Haki ya kulindwa
  2. Haki ya elimu [ ]
  3. Haki ya kusikilizwa
  4. Haki ya kuthaminiwa

iii. Sayansi na Teknolojia ya kutengeneza moto iligundulika katika kipindi kipi kati ya hivi vifuatavyo?

  1. Zama za mawe za kati
  2. Zama za mawe za mwanzo. [ ]
  3. Zama za mawe za mwisho
  4. Zama za mawe za chuma

v. Matendo gani kati ya haya SI wajibu wa mtoto?

  1. Kufanya usafi binafsi wa mwili na nguo zake
  2. Kutafuta kipato kwa ajili ya familia yake. [ ]
  3. Kufanya usafi wa mahali alipolia chakula
  4. Kusaidia wazazi na walezi kufanya kazi mbalimbali

vi. Kiongozi bora ni yule anayefuata misingi na maadili ya uongozi. Je kipi kati ya vifuatavyo si maadili ya uongozi?

  1. Uadilifu
  2. Ukweli na uwazi. [ ]
  3. Uaminifu
  4. Rushwa

2. Oanisha sentensi zilizopo katika sehemu A na maneno yaliyo katika sehemu B ili kupata maana kamili kisha andika herufi ya jibu sahihi katika nafasi ya majibu.

S/N

SEHEMU A

SEHEMU B

i

Makumbusho ya vita vya majimaji

A. Olduvai Gorge

B. Maarifa na ujuzi wa asili katika ususi, ufinyanzi na uhunzi

C. Kilwa kivinje

D. Ulimbombo na ulindi

E. Ngororo kreta

F. Songea

G. Nyumba ya msonge

ii

Vijiti vilivyotumika kupekechwa katika ugunduzi wa moto

iii

Kugundulika kwa masalia ya binadamu wa kale

iv

Jamii za maeneo ya Karagwe, Ufipa na

Ugweno

v

Zina umbo la duara juu na chini

3. Chagua jibu sahihi kutoka katika kisanduku kisha ujaze katika nafasi zilizoachwa wazi.

Koo, Desturi, Pembe za mifugo, Familia, Mila, Pembe za ndovu, Rubega, Jando, Unyago

i. _________________________________________ zilitoka sehemu za mikoa yenye mbuga za wanyama na kupelekwa pwani ya bahari ya Hindi.

ii. Taratibu za kimaisha za mwenendo wa kufanya mambo zinazofuatwa na jamii fulani huitwa.____________________________________________________ 

iii. Vazi maalum linalovaliwa na kabila la wamasai hujulikana kama____________________________________________________ 

iv. Mafundisho ya maadili na afya ya uzazi waliopatiwa vijana wa kiume yalitambulika kama____________________________________________________

v. Familia au jamaa zenye uhusiano wa damu huitwa ________________________________ 

SEHEMU B (ALAMA 20)

4. Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kuandika (UHUSIANO MWEMA au UHUSIANO MBAYA) katika maswali yafuatayo.

i. Kumsaidia mwanafunzi mlemavu kusukuma kiti chake ________________________________ 

ii. Kutowaheshimu vikongwe __________________________________________ 

iii. Kusalimia wakubwa na kusaidia wazazi nyumbani _______________________________________ 

iv. Uhodari wa kucheza peke yako na kujipendelea ___________________________________

 v. Kushiriki kufanya usafi darasani ___________________________________________

5. SOMA HABARI IFUATAYO KWA MAKINI KISHA JIBU MASWALI YANAYOFUATA.

 Zama za Mawe zilihusisha maendeleo ya binadamu kulingana na matumizi ya mawe kama nyenzo kuu ya kutengeneza zana. Zama hizo ziligawanyika katika makundi matatu; Zama za mawe za kale, ambapo watu waliishi kwa uwindaji na kuokota matunda, wakitumia zana za mawe zilizochongwa kwa urahisi. Zama za mawe za kati; kulikuwa na maendeleo katika zana na mbinu za uwindaji, utengenezaji wa nguo kwa kutumia ngozi na magome ya miti.Pia binadamu aligundua moto katika zama hizi. Katika zama za mawe za mwisho, watu walihamia kwenye kilimo, ufugaji na makazi ya kudumu na zana zao zilikuwa bora zaidi. Baada ya zama za mawe kulifuata zama za chuma; ambapo binadamu walijifunza kuyeyusha madini kama vile shaba ikifuatiwa na chuma, wakiboresha zana na silaha mbalimbali na kusababisha maendeleo makubwa katika uzalishaji wao.

MASWALI

i. Zama za mawe ziligawanyika katika sehemu kuu ngapi? ____________________________

 ii. Binadamu alitengeneza nguo kwa kutumia nini? ______________ na __________________

 iii. Maendeleo makubwa yaliyotokea katika zama za mawe za mwisho ni Kilimo, ufugaji na______________________________________

 iv. Ni zama zipi zilikuja baada ya zama za mawe? ___________________________________

v. Katika zama zipi binadamu aliishi kwa kuokota matunda? ___________________________

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD FOUR EXAM SERIES 123

Jina la Mwanafunzi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

Shule . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS UTAWALA WA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

MKOA WA DODOMA 

MTIHANI WA MUHULA DARASA LA NNE

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI [06E]

MUDA : Saa 1:30

MAELEKEZO:

  1. Mtihani huu una maswali sita (6) yenye sehemu A na B
  2. Jibu maswali yote kwenye sehemu zote
  3. Andika majibu yote katika nafasi ulizopewa
  4. Majibu yote lazima yaandikwe kwa kutumia kalamu ya wino mweusi au bluu.
  5. Simu za mkononi au nyenzo yoyote hairuhusiwi katika chumba cha mtihani.
  6. Andika jina na namba ya mtihani katika kila ukurasa wa mtihani huu.
KWA MATUMIZI YA WATAHINI TU
Namba ya Swali Alama Sahihi ya Mtahini Sahihi ya Mhakiki
1.


2.


3.


4.


5.


6.


JUMLA


SEHEMU A: (ALAMA 26)

1. Chagua herufi ya jibu sahihi kisha ujaze kwenye kisanduku ulichopewa

i. Kitendo cha kutoa au kupokea kitu chochote kwa lengo la kupewa upendeleo katika jambo fulani au kupata huduma fulani huitwaje? [      ]

A. Zawadi C. Nidhamu B. Rushwa D. Msaada

ii. Tanzania ni nchi iliyoundwa na mataifa mawili; Tanganyika na Zanzibar. Ni lini muungano wan chi hizo ulifanyika?

A. 9/12/1961 C. 14/10/1999 B. 26/12/1964 D. 26/4/1964

iii. Ipi miongoni mwa tabia zifuatazo huonyesha kitendo cha heshima?

  1. Kumpisha mkubwa kukalia kiti kwenye gari 
  2. Kukataa kuagizwa na mkubwa wako 
  3. Kucheza na wanyama
  4. Kutumia lugha mbaya

iv. Katika historia ya Tanzania, Ni mreno gani wa kwanza kuingia pwani ya Afrika Mashariki?

  1. Mwl. J.K. Nyerere 
  2. Dr. Louis Leakey 
  3. Vasco da Gama
  4. Sultan Seyyid Said

v. Kitu chochote ambacho mtu anastahili kupewa huitwaje?

A. Haki C. Mali B. Wajibu D. Majukumu

2. Oanisha maelezo yaliyopo kwenye orodha A na majibu yaliyopo kwenye orodha B, na kisha uandike herufi ya jibu sahihi kwenye chumba ulichopewa.

ORODHA A MAJIBU ORODHA B
(i) Majengo ya zamani yaliyobaki kama sehemu ya historia na utamaduni.
  1. Makavanzi
  2. Makumbusho
  3. Masimulizi
  4. Maeneo ya kiakiolojia
  5. Magofu

(ii) Sehemu ambapo nyaraka na taarifa mbalimbali za kihistoria huhifadhiwa.
(iii) Maeneo yanapopatikana masalia ya mambo ya kale na utamaduni wa mwanadamu.
(iv) Maeneo yanayotumiwa kuhifadhi vitu vyenye historia na urithi wa kiasili na kiutamaduni.

3. Chagua jibu sahihi kutoka kwenye kisanduku kasha jibu maswali yanayofuata;

Kaole, Zanzibar, Olduvai Gerge, Zinjanthropus, Link

(i) Mji palipogundulika mabaki ya Dinosaria wa Tendaguru.

image

(ii) Sehemu ambapo lipo jengo la maajabu ambalo lina historia ya kuwa jengo la kwanza kuwekwa lifti za umeme.

image

(iii) Eneo lilipogunduliwa fuvu la Binadamu wa kale na Dr. Louis Leakey.

image

(iv) Jina lilopewa fuvu la binadamu wa kale lililogunduliwa mwaka 1959.

image

(v) Mji yanapopatikana magofu ya msikiti na kituo cha kuhifadhia watumwa.

image

SEHEMU B: (ALAMA 24)

4.  Ainisha matendo yafuatayo kwa kusoma maelezo yake na kuweka alama ya vema (√) katika chumba sahihi. Kipengele cha tano (v) kimefanywa kama mfano kwa ajili yako.

Kitendo

Kitendo cha kimaadili

Kitendo kisicho cha kimaadili

(i) Kupigana na wenzako



(ii) Kusalimia watu wakubwa



(iii) Kushirikiana na watu wengine



(iv) Kuwatukana watu wazima



(v) Kumsaidia mzee kubeba mizigo


5.  Tazama picha hizi kwa makini kasha jibu maswali yanayofuata

Maswali

i. Mwanamke aliyeoneshwa katika picha A anafanya nini?

image

ii. Mwanaume anayeonekana kwenye picha B anafanya nini?

image

iii. Jamii ya mtu aliyeoneshwa kwenye picha B hupendelea kula chakula gani.

image

iv. Aina ya nguo aliyoivaa mtu aliyeoneshwa kwenye picha B inaitwaje?

image

6. Soma habari ifuatayo kasha ujibu maswali yanayofuata;

Jamii za Tanzania hapo Kale zilifanya biashara na wafanyabiashara kutoka Mashariki ya Mbali na ya Kati. Nchi hizo ni India, Irani, Iraki, Kuwait, China na Saud Arabia. Biashara hii ilifanyika katika miji iliyopo katika mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi kama vile Dar es Salaam, Bagamoyo, Tanga, Kilwa na Zanzibar. Biashara hizi zilifanyika kwa kubadilishana bidhaa. Bidhaa kubwa katika biashara hii kutoka nchini ilikuwa dhahabu na pembe za ndovu. Dhahabu ilitoka Zimbabwe kupitia bandari ya Sofala, Msumbiji. Kutoka kwa wageni kuja nchini, bidhaa kubwa zilikuwa shanga na vyombo vya ndani kama vile mabakuli na sahani za udongo. Baadhi ya mabaki ya bidhaa hizi yapo katika Makumbusho hapa nchini, kama vile makumbusho ndogo iliyopo Kaole, Bagamoyo.

Maswali

(i) Mabaki ya bidhaa zilizotumika katika biashara na watu wa Mashariki ya mbali zimehifadhiwa wapi?

image

(ii) Taja bidhaa mbili zilizokuwa zinaletwa kutoka kwa wageni?

image

(iii) Tja nchi mbili za Mashariki ya mbali zilizotajwa kwenye habari hii?

image

(iv) Taja miji miwili iliyopo katika Mwambao wa Pwani

image


LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD FOUR EXAM SERIES 114

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

JARIBIO LA NUSU MUHULA-MACHI 2025 DARASA LA NNE

SOMO: HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

DARASA LA NNE

SEHEMU A: CHAGUA HERUFI YA JIBU SAHIHI

1. Chagua herufi ya jibu sahihi kisha iandike kisanduku cha kujibia 

i. Zifuatazo ni haki za mtoto isipokuwa  

(A) kupata elimu bora 

(B) kutomsikiliza anapohitaji msaada 

(C) kupata nafasi ya kucheza 

ii. Kwa majibu wa sheria ya mtoto ni mtu mwenye umri wa miaka rningapi? 

(A) chini ya miaka 10 

(B) chini ya miaka 18 

(C) chini ya miaka 21 

(D) chini ya miaka 15 

iii. Mfumo wa uongozi wa usultani ulitumika katika maneno gani? 

(A) visiwa vya zanzibari

 (B) kaskazini mwa Tanzania 

(C) kusini magharibi mwa Tanzania 

(D) maeneo ya ziwa Tanganyika  

iv. Familia ya mzee lazier na ile ya mzee moleli zina uhusiano wa damu, kipi ni ukweli kuhusu familia.hizi? 

(A) asili yake ni ukoo mmoja 

(B) zinapatikana kutoka jamu ya kisultani 

(C) kiongozi wake ni mtemi 

(D) zinatokana na makabila tofauti 

 

v. Mtemi alikwa na majukumu yafuatayo isipokuwa  

(A) kusimamia ibada za jamii 

(B) kutengeneza zana za chuma 

(C) kuhusisha migogoro katika jamii 

(D) kusimamia biashara katika himaya yake  

2. Oanisha kufungu cha maneno ya kifungu A dhidi ya kifungu cha maneno ya sehemu B kisha uandike herufi ya jibu sahihi katika mabano.

KIFUNGU A

KIFUNGU B

i. Wahehe 

ii. Wamasai 

iii. Wanyamwezi 

iv. Wahaya 

v. Wachaga

A. Mtemi 

B. Mtwa 

C. Mangi 

D. Omukama 

E. laiboni 

 3. Jaza nafasi zilizo wazi kwa kuchagua jibu sahihi kutoka kwenye kisanduku cha majibu. 

Akiologia

Kusimulia

2009

2019

Usultani

Ustawi wa jamii

Ukoo

Kitemi

 i. Kundi la watu wenye nasaba moja, wakijumlisha familia zenye uhusiano wa damu huitwaje?  

ii. Mfumo wa uongozi wa jadi ulioshamiri zaidi katika visiwa vya unguja na pemba uliitwaje  ........................................................

iii. Sheria ya mtoto ilitungwa mwaka  ........................................................

iv. Mtoto ambaye Haki zake zimekiukwa anaweza kwenda kutoa taarifa kwenye ofisi ya  ........................................................ 

v. Je, ni nini maana ya kuelezea jambo au habari kulingana na mlolongo wa matukio?  

SEHEMU B: MAJIBU MAFUPI

4. Kamilisha jedwali lifuatalo kwa kuandika mkoa ambao eneo Ia kihistoria linapatikana. 

Eneo la kihistoria

Eneo na mkoa ilipo

i. Magofu_ya husuni kubwa

 

ii. Gofu la ngome ya gereza

 

iii. Jumba la caravan serai 

 

iv. Gofu la msitiki mkuu

 

 5. Chunguza picha kisha jibu maswali yanayofuata 

(a) Watu wanaonekana katika picha wametoka kufanya shughuli gani? 

(b) Jaza zana mbili za chuma waliotumia watu wa jamii hii kufanyja shughuli hizo 

(i) ........................................................

(ii) ........................................................

(iii) ........................................................

(c) Taja malighafi iliyotumika kutengeneza nguo walizovaa watu wanaonekana katika picha ........................................................ 

(d) Unafikiri hawa ni wa kabila gani hapa Tanzania? 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD FOUR EXAM SERIES 113

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256