JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
MTIHANI WA KUHITIMU KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)
Muda: Saa 3 Mwaka: 2025
Maelekezo
Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali mawili (2) kutoka sehemu C ambapo swali la tisa (9) ni la lazima.
Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelathini (30).
Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.
SEHEMU A (Alama 16)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Katika vipengele (i) hadi (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu chako cha kujibia.
(i) Ni taarifa zipi zinazoandikwa kupatikana katika kamusi kati ya hizi?
Neno, maana, matumizi na matamshi ya semi
Maana, neno, mazungumzo na matumizi ya semi
Matamshi ya semi, matamshi, maana na mazungumzo
Matamshi, mazungumzo, maana na kidahizo
Kidahizo, matamshi, mazungumzo na semi
Choose Answer :
(ii) “Juma anaendesha baiskeli yake polepole.” Kiarifu cha sentensi hii kimejengwa na mfuatano upi wa vipashio?
Kiima, chagizo na shamirisho
Kitenzi kshirikishi, shamirisho na chagizo
Kiarifu, kiima na chagizo
Shamirisho, chagizo na kitenzi kikuu
Kitenzi kikuu, shamirisho na chagizo
Choose Answer :
(iii) “Tutakuja kumpokea kwenye uwanja wa ndege.” Kazi ya kielezi kinachojitokeza kwenye sentensi hii ni ipi kati ya hizi?
Kueleza idadi
Kueleza mahali
Kueleza namna
Kueleza wakati
Kueleza nafsi
Choose Answer :
(iv) Tamathali ipi ya semi hufanisha mambo kwa kutumia viunganishi?
Tashititi
Sitiari
Nidaa
Tashbihi
Tabaini
Choose Answer :
(v) Tamathali ipi ya semi inatawala katika wimbo ufuatao?
Ze ndi ndi ndi!
Tolly ndi!
Ndi ndi ndi ndi!
Tolly ndi! ×4
Tabaini
Taniaba
Tashbihi
Takriri
Tashihisi
Choose Answer :
(vi) Neno lipi linadhihirisha kauli ya kutendeka katika kitenzi pika?
Pikia
Pikiwa
Pikika
Pikwa
Pikisha
Choose Answer :
(vii) Yupi kati ya watafiti wanaojishughulisha na kusoma, kuchambua na kutoa maoni katika kazi za sanaa?
Mdhamini
Mtunzi
Mhariri
Msomaji
Mhakiki
Choose Answer :
(viii) Hatua mojawapo ya uendelezaji wa lugha ili itumike kitaifa na kimataifa ni kuisanifisha. Jambo lipi kubwa linalofanywa katika hatua hii kati ya yafuatayo?
Kupunguza maneno ya kukopa
Kuondoa tofauti za kimsamiati
Kuifanya itumike na jamii ndogo
Kuweka tofauti za kimatamshi
Kuidhinisha tofauti za maneno
Choose Answer :
(ix) Ni kwa namna gani tungo hutofautiana na sentensi?
Tungo zote ni sentensi lakini sentensi zote si tungo
Sentensi haitoi taarifa kamili lakini tungo hutoa taarifa kamili
Sentensi ni miongoni mwa tungo lakini si kila tungo ni sentensi
Tungo sharti ikamilike lakini sentensi si lazima ikamilike
Tungo ni ndefu sana lakini sentensi ni fupi sana
Choose Answer :
2. Oanisha mifano ya tamathali za semi iliyo katika Orodha A na tamathali husika zilizo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kijitabu chako cha kujibia.
Orodha A
Orodha B
Kilio cha mama mfiwa kilisikika mithili ya king’ora.
Haba na haba hujaza kibaba.
Misitu ni uhai.
Shughuli zimejifungua salama.
Upepo mkali ulipiga mluz(i) kila ulipogonga kingo za mito.
8. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata. Kwa hakika mwaka ule watu walinuna sana. Haikuwahi kutokea karibuni kwa kipindi cha muongo mmoja hivi kuwa na mvutano wa kisiasa hicho. Maghala yalijaa mahindi, mtama, mpunga, uwele, maharawe, njegere na njugumawake. Nyama nyingi ziliileta kutoka porini ambapo wanawake walizisanda na kuzikauusha motoni. Aidha, samaki wakubwa wakubwa walipatikana kwa wingi, samaki ambao hawakuwahi kupatikana hapo awali. Kila mmoja kijijini hapo alikuawa na furaha.
Mavuno hayo yaliambatana na sherehe za mwisho wa mwaka ambazo zilikuwa ni zenye kufurahisha. Vigelegele vilisikika, ngoma zilipigwa na marimba yakavuma kijijini huku watu wa rika zote wakicheza bila kujali kuwa ni wazee au watoto. Wasichana wa umri wa miaka kulekulea kumi na mbili walitikisa miili yao kwa mvuto, huku miguu yao ikifuata mitindo maalumu kutoka andani ngoma yenye vumbi, wakicheza kwa madaido wakizungusha shingo zao kama twiga mbugani. Walipeana zamu ya kucheza wengine wakiwa wawili na wengine watatuwatu. Baadaye, wavulana nao waliwezaa ngoma yao. Kadiri ngoma zilivyoundwa, ndivyo vijana waliwyokuwa wakicheza na kuruka juu kama swala. Wazee walitazama na kuridhika huku wanawake wakishangilia kwa vigelegele wakati vijana walioishiwa pumzi wakiondoka jukwaani.
Wakati wanawake na vijana wakicheza na kuimba, wazee walileta kando ya moto wakinywa sharubati mpya. Mmoja baada ya mwingine, wazee hao walisisimama na kuanza kucheza. Wakaijarisha vija kwa mara nyingi tena. Inaga hawakuwa na kasi kama vijana, lakini waliwapiku katika mvuto na ubunifu wa uchezaji wao.
Wapigaji watatu wa marimba walijitokeza na kuonyesha umahiri wao. Kila mpigaji alionesha uhodari wake wa kupiga marimba, kuimba na kucheza. Alipoacha, mwingine alijitokeza, akiimba na kujiunga na tungo iliyoanzishwa. Walikuwa kama kundi la muziki wa wapiga marimba ambao kila aliyekasikia alitviwa na upigaji wa marimba yao uliomliza moyo wa mwayo hadi ndani ya moyo wake. Pangoni. Mdondo wa mziki wa marimba uliingia mwilini mwa mmoja hadi ndani ya moiyo yao.
Wakati wa machweo, watu walipunzwa na kula chakula. Wapiga marimba waliungana na wapiga ngoma na huku na nyimbo za huo uchezi uliendelea tena hadi usiku wa manane. Kilichowandoa watu uwanjani pale ni ama uchovu au usingizi.
Maswali
(a) Andika kichwa cha habari uliyoisoma kisichopungua maneno matatu na kisichozidi maneno matano.
(b) Bainisha shughuli mbili muhimu zilizokuwa zikiwapitia watu riziki kulingana na habari uliyoisoma.
(c) Fafanua kwa kifupi maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika habari uliyoisoma:
Muongo mmoja
Walivapipiku
(d) Fupisha habari hii kwa maneno yasiyopungua mia moja (100) na yasiyozidi mia na tano (105).
10. Lengo kuu la kazi za fasihi ni kuonya na kuisaza jamii. Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila riwaya kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.
11. “Uzembe ni jambo linalokwamisha maendeleo ya jamii nchini Tanzania.” Tathmini kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila tamthiliya kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma.